Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Namna utakavyoifaidi albamu ya Joh Makini ‘God Engineering’

969 26152214 2020089281613826 5015932987481522176 N E1514901170389 TZW

Tue, 2 Jan 2018 Chanzo: bongo5.com

Msanii wa muziki wa hip hop Bongo, Joh Makini amefunguka jinsi mashabiki wake watavyoifurahia albamu yake mpya inayokuja, God Engineering.

Joh Makini ameiambia XXL ya Clouds Fm kuwa katika utoaji wa albamu hiyo kutakuwa na vitu viwili; mosi, albamu yenyewe na The Best of Joh Makini.

“Kuna kitu kimoja nimekisema kwenye huu mfumo wa uuzaji wa albamu, kuna CD itakuwa ya albamu ya Joh Makini inaitwa God Engineering. Halafu kuna The Best of Joh Makini ya ngoma zile ambazo zilitoka lakini bado watu wanakiu ya kuzisikiliza, hizo pia zitakuwa kwenye CD yake,” amesema.

Rapper huyo kutoka kundi la Weusi kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Mipaka’ ambayo leo ameiachia rasmi katika radio station.

Chanzo: bongo5.com