Hivi karibuni kulifanyika shoo kubwa ya producer maarufu Bongo, S2Kizzy ambayo iliwakutanisha pia mwanamziki Moni Centrozone na ex wake, Official Nai.
Hii ilikuwa ni siku nzuri kwa wawili hao na kuziua zile tofauti zao zote zilizokuwa zinazungumziwa juu yao.
Akipiga stori nasi, mwanadada Nai alisema; "Mimi na Moni tupo safi kabisa, hatuna tofauti yoyote kati yetu, alitaka kunifanya wife material hapo ndio niliposhindwa," alisema Nai.
Aidha, Nai alifunguka kuwa Moni alikuwa akimzuia sana kufanya kazi za muziki wakati wakiwa kwenye mahusiano jambo ambalo lilimfanya kuhisi kama ananyimwa uhuru hivyo akaamua kuachana naye.