Msanii maarufu anayeunda Kundi la Navy Kenzo ambaye pia ni mzalishaji wa muziki (prodyza), Nahreel amesema kuwa wasanii wa muziki duniani wanapiga pesa zaidi kupitia mtandao ya Spotify kuliko mtandao wa YouTube ambao Watanzania wengi ndio wameizoea
"Hiyo ni kweli, hii mitandao inaingiza fedha kuliko YouTube ambapo hadi upate views hadi milioni 10 ndio kidogo unafaidika, lakini Spotify ukipata streams (wasikikilizaji) milioni 1 tu unafaidika vizuri," anasema Nahreel.
Wasanii wengi wa Bongo wamekuwa wakitumia zaidi mitandao wa YouTube, Boomplay na iTunes kuuza nyimbo zao wakati mastaa kutoka Marekani na mataifa mengi ya Ulaya wanatumia zaidi Spotify kuuza kazi zao.