Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mzee Majuto alazwa hospitali ya Muhimbili

1908 Mzee Majuto Akifurahia Ushindi TZW

Thu, 25 Jan 2018 Chanzo: bongo5.com

Mchekeshaji Amri Athuman aka Mzee Majuto Jumatano hii amelazwa katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar es saalam kwa mujibu wa taarifa ya Afisa Habari wa Chama Cha Waigizaji Mkoa wa Kinondoni.



Akiongea na Bongo5 Alhamisi hii Asifa Habari huyo, Masoud kaftany, amesema muigizaji huyo alipelekwa hospitali hapo siku ya jana baada ya kuzidiwa.

“Ni kweli Mzee Majuto anaumwa na sasa hivi tupo naye hapa Muhimbili anaendelea na matibabu,” alisema Masoud kaftany. Kusema anaumwa nini ni mapema zaidi lakini baadae tutatoa taarifa rasmi baada ya kupokea taarifa ya madaktari,”

Afisa huyo amekiomba Chama cha Waigizaji, wadau wa filamu Tanzania na wa Tanzania wote wamuombee muigizaji aweze kupona haraka

Chanzo: bongo5.com