Unaweza ukaona kama masihara lakini ndio ukweli wenyewe! Chawa na mtangazaji maarufu Bongo, Mwijaku amemchana bosi wake huyo kwa kumuambia hana ubosi kihivyo!
Mwijaku amefunguka hayo Agosti 9, 2022 alipokuwa akifanya mahojiano na Bongo Five kuhusu mambo mbalimbali ambapo alipoulizwa kuhusu Zuchu ndipo alipomchana Diamond. “Zuchu ni msanii mzuri lakini tatizo lake ni moja tu, Mwambino (Diamond).
Nimemwambia aachane na Mwambino hata haelewi,” alisema Mwijaku. Mwijaku alipoulizwa na mtangazaji wa Bongo Five kama haoni tatizo kusema hivyo na yule ni bosi wake, akasema bosi hawezi kuwa Diamond.