Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwijaku: Vijana muoe wanawake wasio na tamaa za kijinga

Masanja Mwijaku Fgb Mwijaku: Vijana muoe wanawake wasio na tamaa za kijinga

Tue, 4 Oct 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Baada ya sakata la kujitoa uhai kwa katibu katika kanisa la Feel Free lake mchekeshaji ambaye sasa ni mhubiri Masanja Mkandamizaji, sasa watu wengi wamezamia skendo hiyo na kutolea maoni mseto.

Ikumbukwe zogo zima la katibu huyo kujitoa uhai liligeuka changamano hata zaidi baada yake kuacha barua ambayo alimuandikia mkewe mchungaji Masanja Mkandamizaji na kudhihirisha kwamba anampenda sana na yeye alikuwa analijua hilo na ndio maana wivu wa mapenzi umemfanya kujisafirisha jongomeo.

Baada ya tarifa hizo za mkewe baba mchungaji kutoka kimapenzi na mama kanisa, Masanja alizungumzia suala hilo na kuahidi kuzidi kumpenda mkewe hadi pumzi zake za mwisho licha ya skendo ya kimapenzi na marehemu katibu wa kanisa lao.

Mtangazaji Mwijaku pia hajaachwa nyuma kwani amelizamia na kumwambia Mchungaji pole za dhati kwa matukio yanayozunguka kanisa lake pamoja pia na mke wake kutoka kimapenzi na katibu wa kanisa.

Mwijaku ametumia fursa hiyo kutoa onyo kali kwa watu watakaojaribu kufanya mzaha wa kumtongoza mkewe kuwa atawapiga bomu vibaya sana.

Pia aliwashauri vijana kuoa wanawake wasiokuwa na tamaa za kijinga kama mkewe katika kile kilionekana anamkashfu mke wa Masanja kwa kuhusishwa kimapenzi na katibu wa kanisa lake.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live