MTANGAZAJI, mwigizaji na Mhamasishaji wa Klabu ya Simba, Mwijaku anasema kuwa, baada ya kutajwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, hataki kuendelea kufananishwa na machawa maarufu mjini.
Mwijaku amesema; Sasa hivi huwezi kunifananisha mimi na watu kama kina Aristotee au Baba Levo kwa sababu mimi ni kipenzi cha Mama Samia, Serikali inanijua…”
Hivi karibuni, Rais Samia alipiga simu laivu kuwashukuru watu mbalimbali waliomtakia heri ya kumbukumbuku ya siku yake ya kuzaliwa ambapo alisikika kwenye simu akitaja jina la Mwijaku. Ishu hiyo imemfanya Mwijaku kuvimba na sasa hataki kufananishwa na machawa wenzake mjini.