Kutoka kwenye ukurasa wa Instagram wa Dc wa Instagram @mwijaku Ameandika....
"#UKWELI-Siwezi kupinga ukweli ..! Safari yangu ya kwanza QATAR ( WorldCup ) na malipo yake ndio yalio nifanya ninunue eneo na kuanza safari yangu ya kujenga KASRI langu ( Ndoto yangu )
Ukweli usemwe , Ulinipa rizki kupitia kampuni yako, nami nikaitumia vizuri , sitakii kuwa mchoyo ya kushukuru, nakumbuka tulipokuwa Qatar ulinambia kuwa; "pambana wakati wako huu DC " nami nikaichukua hiyo kauli .
Tarehe 5/01/2024 Nimekamilisha ndoto yangu . Kupitia Kampuni yako ilinipa mkataba zaidi ya miaka miwili na malipo ya kila mwezi na nikatumia kama sehemu ya uwekezaji kwangu .
Nasema Asante MWAMBINO. @diamondplatnumz sitaki kuja kusubiria ukifa au nikifa ndio yasemwe haya . Ulinifaa wakati wa shida na wakati wa mahitaji Muhimu .
Asante kwa @donfumbwe Nakumbuka mzigo ulio nipa magomeni usiku wa saa mbili baada ya kupokea simu toka kwa mwambino ndio ulizaa uwekezaji huuuu . Asante kwako kwa kua hukunizunguusha kunikabidhi haki yangu.
Nimshukuru pia mama mzazi wa MWAMBINO @mama_dangote , ulinipa ushirikiano mkubwa pale QATAR na kunambia fanya kazi uisaidie familia yako na niache CHUKI binafsii . Nika kwambia simchukii MWAMBINO but ni kuchangamsha mitandao yetu . Asante kwa kunielewa mama yangu .
Haya Mengine ya mtandaoni ni sehemu zetu za kunogesha game na kuhakikisha tunapambana kukuza burudani .
Mwenyezi Mungu aendelee kuwapa fikra za kuwasaidia wengine kwa kuwapa kazi na kuwapa usia wa kutumia vizuri vipato wanavyo vipata . Asante kwa hili MWAMBINOOO
Mungu akubariki wewe na kizazi chako . Sema na mimi nakushaurii OA mkubwa wakati wako huu Muoe ZUCHU @officialzuchu ana UPEPOO WAKO