Mtangazaji na mwanamitandao maarufu kama DC wa insta Mwijaku ameshindwa kujizuia kusifia video mpya ya mwanamuziki Diamond Platnumz 'Unachezaje iliyotoka rasmi leo hii saa kadhaa zilizo pita.
Kupitia insta story yake Mwijaku ameshare sehemu ya video hiyo na kuandika ujumbe unao-onesha kukubali video hiyo iliyo ongozwa na director Ivan.
Ikumbukwe kuwa mtangazaji huyo mara kadhaa amekua akimkosoa msanii Diamond Platnumz wazi-wazi, katika kazi zake za muziki na hata maisha binafsi huku akiwasifia Alikiba na Harmonize kuwa wanafanya vizuri na ni wasanii wazuri kulikjo Diamond, lakini tangu Mondi amchukue Mwijaku na kumpa ubalozi wa Wasafi Bet, mambo yamebadilika.