DC wa Insta Mwijaku amemuomba msamaha mama wa Staa wa Muziki Zuchu, Khadija Kopa walipokutana visiwani Zanzibar kwenye tamasha la Kizimkazi.
DC Mwijaku alikuwa kwenye vita ya maneno na Zuchu hivi karibuni na kumhusisha hadi mama yake jambo ambalo lilitafsiriwa kuwa halikuwa la kiungwana na ndipo muigizaji Steve Nyerere alipomsaidia Mwijaku kuhakikisha anamfikia Khadija Kopa na kumuomba radhi.
Mara baada ya msamaha huo kutolewa, kupitia ukurasa wake wa Instagram Mwijaku ameandika...
"Tukutane Peponi wale wenye unyenyekevu kama mimi...! Naitwa DC MWIJAKU kipenzi cha watanzania kwa sasa. Innah Llah Maaswabereeen."