Kutoka kwa Mwanamitindo na Mtengeneza Maudhui kutoka Nchini Kenya Shomarwa amesema mwanaume tajiri ni bora kuliko masikini.
"Nimechumbiana na wanaume matajiri na maskini na ninaweza kukuambia tajiri ni bora zaidi. Wavulana wengi maskini huchumbiana na wewe hadi waweze kumudu aina zao. Tusitukuze umaskini,” alisema Shorn Arwa.
Mbali na hivyo aliendelea kusisitiza jinsi kuoa/kuolewa ukiwa na pesa ni bora kuliko kuolewa kwa mapenzi kwani mapenzi yatafuata wakati tayari mtu ametulia.
“Ukipata mtu ana pesa na wote wawili mko tayari Upendo utakuja njiani," alisema Shomarwa kwenye Interview na Mungai Eve.