Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwanamuziki Marekani awapa wanawake watano ujauzito

Mimba Wanawake Watano Mwanamuziki Marekani awapa wanawake watano ujauzito

Tue, 23 Jan 2024 Chanzo: Mwananchi

Katika hali ya kushangaza, mwanamuziki nchini Marekani, Zeddy Will amewafanyia sherehe wanawake watano aliowapa ujauzito kwa mpigo.

Sherehe hiyo kabla ya mtoto kuzaliwa (Baby Shower) imegeuka gumzo kwenye mitandao ya kijamii, wengi wakihoji ni njia gani ameitumia kuwafanya wanawake hao kuelewana na kukubali kushiriki sherehe hiyo ya pamoja.

Kwa mujibu wa tovuti ya Daily Mail, tukio hilo lilionekana kwa mara ya kwanza kupita mtandao wa kijamii wa Tiktok ambako picha ya mjongeo (video) ilichapishwa na mmoja wa wanawake hao.

Lizzy Ashleigh, ndiye alichapisha video hiyo huku akiweka wazi juu ya sherehe hiyo iliyofanyika Januari 14, 2024.

Mwaliko wa sherehe hiyo ulikuwa umeambatanishwa na maneno yasemayo, "Welcome little Zeddy Wills 1-5."

Wanawake wengine waliopewa ujauzito na mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 22 ni Bonnie B, Jylene Vila, Kay Marie, na Iyanla Kalifa Galletti.

Chanzo: Mwananchi