Mbunge wa Jimbo la Muheza Tanga Mwana Fa hakubaliani na Roma Mkatoliki kwa kitendo cha kumfananisha bondia Mike Tyson na Floyd Mayweather, pia ameeleza kwamba kumfananisha Tyson na Mayweather ni kumkosea Mike Tyson.
Mjadala huo umeibuka mtandao wa Twitter baada ya Roma Mkatoliki kuandika kuwa
"Sema Mayweather anacheza sana na akili zetu hata kama ana rekodi kubwa lakini mimi kwangu sio bondia bora, Mike alikuwa mnyama sana"
Mwana Fa aka-comment kwenye Tweet hiyo ya Roma kwa kuandika "Bwana Ibra kumfananisha Floyd na Mike ni kumkosea heshima “The BaddeTHt man on the planet” Iron Mike kiboko kabisa mzee wangu".