Baada ya remix ya wimbo wa ‘Yule’ kutoka kwa mkongwe wa muziki Bongo #AY na #Marioo kupokelewa vizuri, na sasa Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa, Michezo Mwana FA ametoa maoni yake kuhusu ngoma ya ‘Cinderela’ ya Alikiba.
Kupitia ukurasa wa X (zamani twitter) wa #FA ameshare ujumbe kuwa anadhani kuna msanii anatakiwa kufanya remic ya wimbo huo.
“Kwa maoni yangu kuna mtu (msanii) anatakiwa ku’remix Cinderela” ameandika #MwanaFA
Utakumbuka kuwa wimbo wa #Cinderella ndiyo ngoma ambayo ilimtambulisha #Alikiba kwenye muziki wa Bongo Fleva huku mwaka 2006 aliachia rasmi albumu yake ya kwanza yenye jina la ‘#Cinderella’ ikiwa na nyimbo 15 ambazo zilikubalika zaidi. .