Jana msanii wa Muziki wa Bongo Fleva, Ruby kupitia ukurasa wake wa Instagram aliposti picha ikimuonesha mwenye umbo kubwa tofauti na muonekano wake wa siku zote.
Picha hiyo ambayo ni ya kwanza kwa mwaka 2018 kwa msanii huyo kuonekana, Ruby aliiweka na kuwatakia mashabiki wake Kheri ya Mwaka mpya.
Watu wengi waliotoa maoni kwenye posti hiyo wameonekana kushangaa mabadiliko hayo ya ghafla huku wengine wakidai ametumia dawa za kuongeza makalio wengine wakiamini kuwa ametumia App ku’edit picha hiyo.
utamu_baby Mchina ruby huo yaan unatudangny hvhv wakat ulikua mwembamba kama mwiko Wa pilau