Msanii wa Bongo Movies na mjasiriamali, Rose Alphone 'Muna Love'amesema kuwa kwa sasa anatamani kuzaa mtoto mwingine baada ya kumpoteza yule wa kwanza, Patrcik.
Patrcik alifariki dunia Julai 3, 2023 jijini Nairobi nchini kenya alipokuwa amelazwa Hospitalini akiuguzwa
Kupitia mitandao ya kijamii, Muna ameandika; "Sasa natamani kuwa na mtoto tuenjoy, tuzunguke hii dunia na baba yake huku tukimtukuza Mungu kwa furaha ya uzao.
"Yaani zile hekaheka Airport unamuona baba mtoto wako alivyo bize na mwanae kwenye ndege mmekaa mnamtazazama mtoto mnaenjoy yaani najiona kama kuna kitu namiss ni mtoto, God I trust in you," ameandika Muna Love.