Menu ›
Burudani
Thu, 17 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Unaambiwa ndoa ya msanii Britney Spears na mwanamitindo Sam Asghari imevunjika inasemekana chanzo ni Britney kuwa na mahusiano nje ya ndoa (kucheat) baada ya chanzo cha karibu kusema kuwa Sam kamuomba Britney talaka.
Wanandoa hao walikutana kwa mara ya kwanza kwenye seti ya video ya muziki ya Spears mnamo 2016, na walifunga ndoa na kualika watu katika sherehe ndogo lakini iliyojaa watu maarufu mnamo Juni 2022.
Asghari, 29, alikuwa bega kwa bega na Spears, 41, kipindi anapata matibabu yake ya afya ya akili na mwisho wa uhifadhi wake.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live