Lifestyle

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

SIL

Mtoto wa miaka miwili amuua mama yake kwa bastola

623ecae686a2524d Mtoto wa miaka miwili amuua mama yake kwa bastola

Sun, 17 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mkazi mmoja wa jimbo la Florida nchini Marekani amekamatwa na kushtakiwa kwa mauaji ya mpenzi wake mpenzi wake.

Mtoto huyo alipata bastola hiyo kwenye begi la watoto wakati mama yake alikuwa katika mkutano wa kikazi kupitia video kwenye mtandao wa ZoomKisha mwana huyo alichukua silaha hiyo, akasongea nyuma ya mama yake na kumpiga risasi papo hapo Baba yake mtoto uyo sasa anakabiliwa na mashtaka ya mauaji na kushindwa kutunza silaha hiyo na anaweza kuhukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani.

Hii ni baada ya mtoto wao mwenye umri wa miaka miwili kutekeleza mauaji hayo mnamo Agosti 2021.

Kwa mujibu wa ripoti ya BBC, mwanawe Veondre Avery, 22, alipata bastola kwenye begi la watoto wakati mama yake Shamaya Lynn alikuwa katika mkutano wa kikazi kupitia video kwenye mtandao wa Zoom.

Kulingana na polisi, kisha mwana huyo alichukua silaha hiyo, akasongea nyuma ya mama yake na kumpiga risasi papo hapo.

Mmoja wa wafanyakazi wenzake na Lynn aliyekuwepo kwenye kikao hicho cha Zoom, ndiye alikuwa wa kwana kuwapigia simu watoa huduma za dharura.

Alipiga ripoti kwa polisi kuwa alisikia sauti kubwa na kumuona Lynn akiangukia mgongo.

“Mmoja wa wasichana amezimia….camera yake imewashwa na mtoto wake analia kwa nyuma,” mfanyakazi huyo alisema kwenye simu ambayo polisi waliitoa kwa vyombo vya habari.

Avery ampata mke wake sakafuniGazeti la Orlando Sentinel, linaripoti kuwa Avery aliporejea nyumbani, alimpata mpenzi wake akitokwa na damu akiwa amelala sakafuni.

Aliwafahamisha polisi na kuomba watoa huduma wa dharura kufanya haraka huku akionyeshwa kwenye video ya zoom akifanya huduma ya CPR akisema: "Nimerudi kutoka kazini na sijui kilichotokea."

Maafisa wa kutoa huduma za dharura waliwasili na kujaribu kumsaidia marehemu aliyekuwa na umri wa miaka 21, lakini juhudi zao hazikufua dafu.

Hata hivyo, watoto wengine wawili wa wanandoa hao ambao walikuwa nyumbani hawakujeruhiwa na wanatunzwa na jamaa zao.

UtepetevuAvery sasa anakabiliwa na mashtaka ya mauaji na kushindwa kutunza silaha hiyo na anaweza kuhukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani.

Polisi walisema kuwa bunduki hiyo iliwekwa kiholela kwenye begi la watoto ambalo liliachwa kwenye sakafu chumbani mwa wazazi hao.

Kesi dhidi ya Avery itatajwa tena mnamo Novemba 23, 2021 na bado .

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke