Mtoto wa ‘rapa’ Kanye West, North West amefanikiwa kuingia kwenye chati za Billboard 100 kwa mara ya kwanza, baada ya kufanya 'kolabo' na Baba yake ya ngoma ya ‘Talking’ na kumfanya kuwa miongoni mwa wasanii wenye umri mdogo zaidi kuwahi kuingia katika chati hizo.
Wimbo wa ‘Talking’ mpaka kufikia sasa unazaidi ya watazamaji milioni 14 kupitia mtandao wa #YouTube, huku kwa upande wa #Billboard ngoma hiyo ikishika nafasi ya 30 katika chati hizo.
Kanye alifanikiwa kupata mtoto huyo na aliyekuwa mpenzi wake mfanyabiashara #KimKardashian ambapo mpaka kufikia sasa Binti huyo ana umri wa miaka 10.