FIlamu inayoelezea maisha ya George Floyd, inaendelea kutengenezwa, Kwa mujibu wa variety, Radar Pictures, 8 Queens Film & Media Productions, na Night Fox Entertainment wanatarajia kuachia filamu hiyo inayoitwa “Daddy Changed the World.”
Ambapo Binti wa George GiannaFloyd, na mama yake, Roxie Washington, watakuwa waandaaji wakuu (Executive Producer) wa FIlamu hiyo.
Kama utakumbuka Mei 25, 2020 Mmarekani Mweusi George Floyd aliuawa na afisa polisi mzungu Derek Chauvin, Hivyo FIlamu hiyo imeangazia kuelezea maisha ya Floyd kama baba ambaye kifo chake kilibadilisha Ulimwengu na kudai kuleta haki na usawa kwa watu wote.