Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Msanii Ben Paul asaka talaka dhidi ya mkewe Anerlisa Muigai

49c20c60a164b2fa Msanii Ben Paul asaka talaka dhidi ya mkewe Anerlisa Muigai

Thu, 8 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Ben Pol anadaiwa kuwasilisha ombi la talaka katika mahakama ya Mwanzo jijini Dar Es Salaam

- Bado haijafahamika ni lini mwanamuziki huyo aliwasilisha talaka hiyo lakini duru zinaarifu kwamba suala hilo ni la kweli na wala sio kutafuta kiki jinsi wengi wanavyodhani

- Kulingana na Millard Ayo, ulimwengu bado uko njia panda kujaribu kuelewa ni kwanini Ben Pol aliamua kumtaliki mumewe

Mwimbaji wa Tanzania Benard Paul Mnyang’anga anayejulikana kwa jina la Ben Pol ameripotiwa kuwasilisha ombi la talaka dhidi ya mkewe Anerlisa Muigai, TUKO.co.ke imebaini.

Chapisho hili linafahamu kuwa Ben Pol anadaiwa kuwasilisha ombi hilo katika mahakama ya Mwanzo jijini Dar Es Salaam.

Bado haijafahamika ni lini mwanamuziki huyo aliwasilisha talaka hiyo lakini duru zinaarifu kwamba suala hilo ni la kweli na wala sio kutafuta kiki jinsi wengi wanavyodhani.

Kulingana na Millard Ayo, ulimwengu bado uko njia panda kujaribu kuelewa ni kwanini Ben Pol aliamua kumtaliki mumewe.

Ikiwa suala hilo ni la kweli, basi baina ya Ben Pol na Anerlisa huja inawadia yapata mwaka mmoja baada ya wawili hao kufunga ndoa.

Kama ilivyoripotiwa hapo awali na TUKO.co.ke, Anerlisa na Ben Pol walifanya harusi kubwa na ya kifahari iliyojaa usiri mno kule Tanzania mnamo Mei 2020.

Awali, TUKO.co.ke iliripoti jinsi mahabuibu hao wawili walibadilishana pete katika Kanisa la Katoliki la St. Mbezi Beach jijini Dar Es Salaam.

Harusi yao ilihudhuriwa na ndugu, jamaa na marafiki wa karibu sana wa wapenzi hao.

TUKO.co.ke aidha inafahamu fika kwamba Ben Pol wala Anerlisa hajatoa taarifa yoyote hadharani kuhusiana na talaka hiyo.

Hata hivyo, Anerlisa aliashiria kuna jambo baada ya kuzifuta piccha zote aliopiga akiwa na mumewe Ben Pol na vile vile kubadilisha jina lake kuwa Anerlisa Muigai kutoka kwa Anerlisa Muigai Mnyang'anga.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke