Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mrisho Mpoto ahoji wasanii maarufu kuoa nje, ‘kuna tatizo wanahitaji kufundwa’

8426 26872054 1883151778642688 5664516741879824384 N TZW

Mon, 28 May 2018 Chanzo: bongo5.com

/>

Kauli ya Mpoto amekuja pale alipoeleza kuwa awali alishauriwa na Harmonize video hiyo ikafanyike Nigeria au Afrika Kusini ila akakataa kutokana ujumbe wa wimbo huo ni kwa ajili ya Watanzania.

“Kwa sababu wimbo mimi naongea na Watanzania, nilikuwa nimeguswa na jinsi vijana wetu wa Kitanzania wanavyokwenda kuoa nje ya Tanzania, kwa nini vijana wetu maarufu hawataki kuoa nyumbani?,” alihoji.

“Nikaliona hilo, nikajua kuna tatizo hapa, hawa wanahitaji kufundwa, hawa kuna maneno wanatakiwa kuambiwa, waambie na mwenye maneno yake,” Mpoto ameiambia Times FM.

Katika hatua nyingine amesema kuwa licha ya video hiyo kufanyika Bongo, pia Harmonize amechangia karibia asilimia 40 ya bajeti yake na sehemu iliyobaki akamalizia yeye pamoja na wadau.

Loading...
Chanzo: bongo5.com