Mrembo mmoja amesimulia jinsi kumfumania mama yake akishiriki tendo la ndoa na mwanamume mwingine kulivyomuathiri utoto wake na sasa alifichua hayo ili kupata uponyaji.
Alisema hayo yalitokea akiwa na umri wa miaka sita na bado anaishi na kumbukumbu hilo hadi sasa. Mwanamke huyo alichora picha waziwazi, akionyesha kwamba alijua kilichotokea wakati huo.
"Mama yangu ni mke asiye mwaminifu. Nilimfumania akishiriki ngono na mwanaume mwingine, akatuweka chini na mdogo wangu."
Mwanamke huyo aliendelea kufafania akisema kuwa chochote kinachomtokea mtoto wakati akikua kinaweza kuchochea kwa muda mrefu juu jinsi maisha yake yake ya baadaye yatakavyokuwa.
"Lolote litakalotokea kwa mtoto ambalo ni baya, huwa halisahau. Lakini inawezekana kwamba ikiwa ni jambo jema, anaweza kusahau."
Alipoulizwa iwapo taa ilikuwa imezimwa wakati wa tukio hilo alisema: "Taa ya kando ya kitanda ilikuwa imewaka. Ndugu yangu mdogo alikuwa amelala kando yangu sakafuni; bado nilikuwa nakumbuka."