Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mr Blue ajivunia `mdomo’ wake

E5526dcfecfe6896bd7d736a475e019a Mr Blue ajivunia `mdomo’ wake

Mon, 31 Aug 2020 Chanzo: habarileo.co.tz

NYOTA wa muziki wa kizazi kipya Khery Rajab ‘Mr Blue’ amesema licha ya kupata ajali na kuteguka mkono, bado ana uwezo wa kuendelea kufanya ‘show’ kama kawaida .

Mr Blue aliyeumia akiwa kazini tangu wiki mbili zilizopita alisema bado anajivunia baada ya mdomo wake haujaumia na ni chombo anachotumia kutoa mistari hivyo kiafya yupo sawa kwa kufanya shoo ili kuwapa burudani mashabiki na wapenzi wa muziki huo.

Msanii huyo alitoa kauli hiyo juzi mjini Tanga alikoenda kufanya onesho lililofanyika kwenye ukumbi wa Sabasaba iliyoandaliwa na kudhaminiwa na Kampuni ya Katemi Empire.

“Ni kweli nimeumia lakini sijavunjika, ila nimeteguka nikiwa kazini, sasa siwezi kusema sitafanya shoo, kwani mdomo, ambao ni chombo ninachotumia kutoa mistari kipo salama, “ alisema Mr Blue.

Alisema kwenye kila shoo au tamasha linalofanyika kunakuwa na usalama, hivyo anajivunia hicho na kuendelea kupata nguvu ya kutoa burudani ya kuwaburudisha mashabiki wake wa muda wote.

Chanzo: habarileo.co.tz