Menu ›
Burudani
Fri, 30 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Babylon Bizzy Mr Blue amefunguka kupitia The Switch kuwa skendo iliyowahi kumshtua sana ni ile ya kutangaziwa kuwa amekufa.
“Walitangaza kuwa Mimi NIMEKUFA, ilinitisha sana ile skendo, nikaona imekuwaje mpaka wanataka waniue Sasa, yaani wamesema mpaka waniue.
“Ilikuwa kama miaka 10 iliyopita nilikua narudi kutoka Kenya, ilitangazwa kuwa nimepigwa bastola Kinondoni. Mama aliangaika halafu kwenye simu hanipati, Sasa wakati Narudi namkuta mama yupo karibu na nyumbani anatembea kama mtu aliyekata tamaa.”
Chanzo: www.tanzaniaweb.live