Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

“Movie ya dakika 60 tumeshindwa, je tunapokimbilia tutapaweza?”-Kitale

1237 Z1 660x400 TZW

Sun, 7 Jan 2018 Chanzo: millardayo.com

Muigizaji na mchekeshaji Mkude Simba ambaye wengine wanamfahamu kama Kitale kutokana kujipatia umaarufu kupitia tamthilia ya Jumba la Dhahabu, Kitale ameamua kutumia ukurasa wake wa isntagram na kueleza mawazo yake baada ya wasanii kushindwa kufanya vizuri kwenye movie na wengine wamerudi kwenye tamthiliya.

“Hii ni kwa wasanii wenzangu. Soko letu la movie kipindi Cha nyuma lilitokea kupendwa na mashabiki zetu wengi sana tena sana, hapa kati kati kulitokea songombingo nyingi sana juu ya soko letu la film bongo kuporomoka kutokana na kazi zetu kuwa chini ya kiwango”

“Mashabiki zetu ambao ndio wanunuzi wa kazi zetu walihamia katika series za kikorea, Baadhi ya wasanii waliyumba sana kutokana na tegemezi lao kubwa lilikuwa kwenye biashara ya movie tu. Kama tutakuwa tunafuatilia vizur sasa hivi wasanii wengi tumejikita katika TAMTHILIA (Series)”

“Shaka yangu Bongo movie tumeiuwa sisi wenyewe kutokana na Story zetu mbovu, huku tulipokimbilia ni pagumu zaidi ya movie na ikumbukwe kua tamthilia ni story ndefu huenda hata mwaka au zaidi ya mwaka kutokana na ww mwenyewe upendavyo kulingana na story”

“Pia inahitaji watu wengi tofauti na movie. Swali Langu, “Movie ya dakika 60 tumeshindwa, Je huku tunapokimbilia tutapaweza ikiwa Tamthilia ni zaidi ya dakika 60.?” Tusije tukaharibu kotekote tukaja kosa kote..!! Ingawaje Nina Imani tunaweza”

“Tunakabiliana nao vp wale waliosababisha kuonekana Hatuwezi..??? Maana SAMAKI mmoja alivyooza kule kwenye Movie tulijumrishwa wote. Mmmh..!!! Lakini Haya yote ni Maneno ya Kuambiwa”

Video iliyowanasa Dogo Janja na Irene Uwoya wakipelekana saloon

Chanzo: millardayo.com