Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Motra The Future atoa siri ya kufanya remix ya Waka kutoka kwa Diamond (+audio)

3776 Asasasasas TZW

Tue, 27 Feb 2018 Chanzo: bongo5.com

Msanii wa muziki Bongo, Motra The Future amefunguka sababu ya kufanya remix ya ngoma ya Diamond ‘Waka’ ambayo muimbaji huyo amemshirikisha Rick Ross.



Motra ameiambia Bongo5 sababu ya kufanya remix ya ngoma hiyo ni kumbumbusha Diamond kuhusu kauli yake aliyotoa kuwa moja marapa ambao anatamani kufanya nao ngoma ni Motra The Future.

“Nilifanya vile kama statement ya kumkumbusha kuhusiana na kauli yake ambayo aliitoa lakini kwa sababu najua ni brother mishe nyingi, yupo bize nikaona nitengeneze ili atatakaposikia akumbuke,” amesema Motra.

Pia amesema kuhusu kufanya video ya ngoma hiyo ni hadi pale atakapowasiliana na uongozi wa Diamond. Katika Hatua  nyingine Motra amezungumzia ngoma yake mpya ‘Mwajuma chaUtudu’.

Msikilize hapa.

Chanzo: bongo5.com