Menu ›
Burudani
Wed, 10 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Msanii maarufu wa muziki wa rap nchini Tanzania, Awadhi Chami anafahamika zaidi kama Moni Centrozone ametangaza kuachana na kazi ya muziki mara tu atakapoitoa Album yake ya mwisho.
Moni ambaye anatokea Kanda ya Kati nikimanisha Dodoma, amethibitisha hilo kupitia WhatsApp status yake kwa kuandika maneno haya;
"Album moja kabla sijastaafu muziki rasmi. Imekuwa ni safari ndedu tangu nilipokuwa mtoto, nimeuweka mji wangu Kwenye Ramani," ameandika Moni Centrozone.
Je, Unatamani Moni Centrozone aache muziki?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live