Rapa anayewakilisha pande za 'Dom Town' Mji Mkuu hapa nchini Tanzania, Dodoma Moni Centrozone ameshea orodha ya wasanii wake 10 anaowakubali kwenye upande wa muziki wa HipHop lakini cha ajabu hajamuweka mshkaji wake Country Wizzy.
Submitted by Shaluwa Anta on Jumanne , 11th Mei , 2021 Picha ya pamoja ya wasanii Country Wizzy kushoto, na Moni Centrozone kulia
Moni Centrozone ameeleza kwamba kwa bara la Africa anamkubali zaidi Jay Moe na dunia kwa ujumla anamkubali rapa J Cole.
Katika orodha yake hiyo ambayo ameiweka kwenye 'Insta Story' yake amewataja wasanii wafuatao
1. J Cole
2. Jay Moe
3. Kendrick Lamar
4. Nas
5. Marehemu Albert Mangwea
6. Marehemu BIG Notorious
7. Jay Z
8. Prof Jay
9. Kanye West
10. Post Malone