Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Model wa video ya ‘Ntampata Wapi’ ya Diamond ashinda taji la Top Model SA

5071 2018 02 20 PHOTO 00000012 750x1000 TZW

Tue, 20 Mar 2018 Chanzo: bongo5.com

Unamfahamu Melissa Magiera ambaye amewahi kuonekana kwenye video ya ‘Ntampata Wapi’ ya Diamond? Nadhani utakuwa umeshamkumbuka kupitia video hiyo niliyokutajia.

                                                    Melissa Magiera

Mrembo huyo ambaye kwa sasa yupo chini ya kampuni ya Fan Jam Model Management, wiki iliyopita amefanikiwa kushinda taji la Top Model 2018 nchini Afrika Kusini.

Melissa ameshinda taji hilo kwa kuwabwaga washiriki wengine 38 ambao walifanikiwa kutinga katika hatua ya nusu fainali.

Mrembo huyo ataiwakilisha Afrika Kusini kwenye mashindano ya Top Model ya dunia ambayo yatafanyika Ijumaa ya April 6 na 7 ya mwaka huu mjini London.

Chanzo: bongo5.com