Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mobetto agoma kumuiga Diamond

Mobeto Mn.jpeg Hamisa Mobeto na Diamond

Sun, 15 May 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Hamisa Mobeto; ni mwanamitindo, muigizaji na msanii wa Bongo Fleva ambaye anasema kuwa wiki ijayo ataachia Extended Playst (EP) yake kisha itafuata albam.

Hamisa amesema; “Wiki ijayo natoa EP yangu, itakuwa ni ya kwanza tangu nimeanza safari yangu ya muziki, tulikuwa tunabishana kati ya kutoa albam au tutoe EP, kwa hiyo naona jambo limekimbilia kwenye EP.”

Alipoulizwa kama ametumia mtindo wa Diamond Platnumz ambaye ameachia EP yake, First of All (FOA) kisha itafuata albam, Hamisa amesema hajui hilo ila EP yake ni mipango ya menejimenti yake.

“Siwezi kujua huko kwingine lakini, tunatumaini kwa hilo kwa sababu nyimbo tunazo nyingi sana na kolabo zipo nyingi sana, kwa hiyo ni sisi tu kuchangua tutoe nini, tuache nini. Kwa hiyo lengo kubwa ni albam, lakini kwa ratiba yetu hairuhusu, hivyo tunatoa EP kwanza,” amesema Hamisa.

Hamisa aliingia rasmi kwenye muziki wa Bongo Fleva mwaka 2018 alipoachia ngoma yake ya kwanza ya Madam Hero.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live