Menu ›
Burudani
Thu, 9 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mpenzi wa zamani wa Tiger Woods, Erica Herman, amefungua kesi Mahakamani akitaka kulipwa Dola Milioni 30 (Tsh bilioni 70), baada ya kufukuzwa nyumbani walipoishi wote kwa takriban miaka 6.
Erica amesema Woods na watu wake walimdangaya ajiandae kwa safari ya peke yake, ambapo walimshusha uwanja wa ndege na kumwambia hawezi kurudi tena nyumbani, pia wakabadilisha vitasa vya nyumba.
Anadai kuwa akiwa nyumbani hapo alimfanyia nyota huyo wa Tennis "huduma za thamani" badala ya kulipa kodi, na pia walikuwa na makubaliano ya mdomo ambayo yangemruhusu kukaa hapo hadi miaka 5 baada ya kuachana.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live