Lifestyle

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

SIL

Mkalimani afunguka "Niliongea mengi mmeliona lile"

MKCC Mkalimani afunguka "Niliongea mengi mmeliona lile"

Fri, 2 Apr 2021 Chanzo: eatv.tv

Mkalimani Matungwa Mutatina aliyezua gumzo mitandaoni siku ya kumuaga Hayati Dkt John Pombe Magufuli Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma, amesema kilichomtokea sio kushindwa kutafsiri maneno bali ni matatizo ya kiufundi.

Submitted by Shaluwa Anta on Alhamisi , 1st Apr , 2021 Picha ya Mkalimani Matungwa Mutatina

Akipiga stori na EATV & EA Radio Digital, Mkalimani huyo amesema mitambo ilifika mahala ambapo sauti inatoka ikiwa inakatakata kisha akawa hasikii kabisa sauti inayotoka kwa aliyekuwa anaongea.

"Ile hali ilinistua kidogo, kilichokuwa kimetokea haikuwa kwamba nimeshindwa kutafsiri maneno ila kulikuwa na sababu za kiufundi, mitambo ilifika mahala ikawa haisikii na sauti inakuja kwa kukatakata lakini haikunivunja moyo, kwa sababu waliokuwa wanacheka hawakujua kilichotokea na kuendelea" ameeleza Mkalimani Matungwa Mutatina 

Aidha Mkalimani amesema anawaomba watu wawe na uzalendo na wajirekibishe kwa kilichotokea kwa sababu kulikuwa na vitu vingi hasa ilikuwa siku ya kumuaga Hayati Dkt John Pombe Magufuli ila watu wamemdhihaki na kumcheka kwa kilichomtokea.

Zaidi mtazame hapa chini.

Chanzo: eatv.tv