Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Miss USA Noelia Voigt ajiuzulu kisa afya ya akili

Miss USA Noelia Voigt Amejiuzulu Cheo Chake, Akitaja Sababu Za Afya Ya Akili Miss USA Noelia Voigt amejiuzulu cheo chake, akitaja sababu za afya ya akili

Wed, 8 May 2024 Chanzo: Bbc

Bi Voigt, ambaye alishinda shindano la kila mwaka mnamo Septemba, alisema anaamini katika kufanya maamuzi "ambayo yanahisi bora kwako na afya yako ya akili".

"Kamwe usihatarishe afya yako ya mwili na kiakili," aliandika kwenye Instagram. "Afya yetu ni utajiri wetu."

Shirika la Miss USA lilisema linaunga mkono uamuzi wake na litatangaza mrithi wake.

Mmarekani huyo wa Venezuela mwenye umri wa miaka 24, alisema kwamba anatumai "kuendelea kuwatia moyo wengine" anapoanza "ukurasa mpya" maishani.

"Tanguliza afya yako ya akili, jitetee mwenyewe na wengine kwa kutumia sauti yako na usiogope kamwe yale yatakayotokea siku za usoni, hata kama unahisi kutokuwa na uhakika," alisema.

Alitoa shukrani zake kwa miezi tisa kama Miss USA, ambayo alisema ilimpa "jukwaa ... kuleta mabadiliko" na pia kutimiza "ndoto ya maisha" na kukutana na "watu duniani kote."

Miss USA alimshukuru Bi Voigt na kusema kwenye Instagram kwamba "afya njema ya washikaji taji ni kupaumbele".

Shirika hilo lilisema linakagua mipango ya "kupitisha majukumu kwa mrithi".

Savannah Gankiewicz wa Hawaii alishika nafasi ya pili baada ya Bi Voigt katika shindano la mwaka jana.

Chanzo: Bbc