Menu ›
Burudani
Thu, 21 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Muigizaji nguli wa Filamu kutoka nchini Tanzania, Jackline Wolper amefunguka ya moyoni kuwa hana maelewano mazuri na mume wake, Rich Mitindo tangu mwaka jana (2023) mwezi Juni.
Wolper kupitia mitandao ya kijamii amefunguka kuwa ni miezi 9 sasa ndoa yake na Rich Mitindo inapumulia mipira.
Aidha, mrembo huyo ambaye ni mama wa watoto wawili, amedai hatoi taarifa zozote kuhusu mume wake kwa sasa kwani wanalea watoto tu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live