Mgahawa wa Guolizhuang unaopatikana Nchini China, katika mji wa Beijing, ni maarufu kwa kutoa huduma ya chakula kilichotengenezwa kwa kutumia sehemu za siri (uzazi) za wanyama mbalimbali.
Na raia wa China wanaamini kuwa sehemu za siri za wanyama husaidia kuongeza nguvu na uwezo wa mwanaume kuzalisha huku pia humsaidia mwanamke kulainisha ngozi yake.
Hata hivyo unaambiwa moja ya kiungo cha siri kinachouzwa kwa gharama kubwa katika mgahawa huo ni uume wa mnyama ajulikanae kama chui ambapo gharama zake zimetajwa kuwa ni Milioni 2.5 kwa pesa za kitanzania.
Pia mgahawa huo hutoa divai yenye chembechembe za damu ya uume na moyo ambayo inasemekana kufanya kazi vizuri zaidi kuliko dawa za kuongeza nguvu za kiume.