Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Meneja afunguka kuhusu wasanii kwenda kwa waganga

Maneno Meneja Maneno

Mon, 26 Jul 2021 Chanzo: eatv.tv

Meneja Maneno amenyoosha maelezo kuhusu stori zinazosemekana kwamba huwa anawapeleka wasanii wake kwa waganga ili waweze ku-hit kwenye muziki kwa kusema watu wanaomsema hivyo wanamkosea na haamini kwenye ushirikina.

"Wananikosea sana mimi namuamini Mungu, isipokuwa kwenye kutafuta maisha kuna njia nyingi kwahiyo inategemea na imani ya mtu lakini siamini kwenye ushirikina kwamba ukifanya hivyo ndio umefanikiwa kwa sababu kuna wasanii wengi wanafanya vizuri na hawajapitia huko" amesema Meneja Maneno 

Meneje Maneno tayari ameshafanya kazi ya kuwasimamia wasanii wakubwa Bongo kama TID, Hemedy PHD, Rich Mavoko, Diamond Platnumz, Ommy Dimpoz na sasa yupo na Sholo Mwamba.

Chanzo: eatv.tv