Rapa maarufu wa Marekani, Robert Rihmeek Williams 'Meek Mill' ameeleza nia yake ya kupata uraia wa nchi ya Ghana.
Kulingana na rapper huyo mzaliwa wa Philadelphia, anataka kutulia Ghana kutokana na ukandamizaji wa Amerika kwa watu weusi.
“Nataka kupata uraia nchini Ghana!!!! Marekani imefanya kuwaangusha watu weusi ikiwa hutafuata amri!” alitweet kwenye chapisho la X mnamo Machi 4, 2024.
Mnamo Desemba 2022, rapper huyo alitumbuiza katika tamasha la muziki la Afro Nation nchini Ghana.
Uwepo wake nchini Ghana ulifikia kilele cha ziara yake katika Jubilee House, ambapo alikutana na kufanya mkutano na Rais Nana Addo Dankwa Akufo-Addo.
Licha ya kuonyesha hasira za umma baada ya kurekodi sehemu za video ya muziki katika kiti cha serikali, Meek Mill, ambaye tangu wakati huo ameomba msamaha kwa Waghana kwa kitendo chake, ameonyesha mapenzi yake kwa Ghana.
Kwa kipindi hicho, ameonyesha nia yake ya kurejea Ghana na kufanya kolabo na baadhi ya wasanii maarufu wa Ghana.
Hivi karibuni Meek Mill amekuwa kwenye mtandao wa kijamii kufuatia madai kuwa alitajwa kwenye kesi iliyofunguliwa na aliyekuwa mfanyakazi wa rapa na prodyuza Sean ‘Diddy’ Combs.
Kulingana na ripoti nyingi, kesi iliyowasilishwa na Rodney "Lil Rod" Jones ilimweka Meek Mill kwenye orodha ya majina yaliyoongezwa kwenye sakata mapenzi ya jinsia moja linalomhusu Diddy.
Lakini katika mfululizo wa machapisho ya X, Meek Mill amekanusha madai hayo huku akigusia njama ya kudhoofisha bidii yake akiwa Mmarekani mweusi.
Meek Mill alitembelea Ghana kwa ziara ya kwanza mnamo Desemba 2022.
I wanna get citizenship in Ghana!!!! America made to tear black men down if you don’t follow orders!
— MeekMill (@MeekMill) March 5, 2024