Mwanamitindo Mtanzania Happy Carter (Mdogo wa Mbwana Samatta) ambaye anafanya poa sana Duniani mwenye makazi nchini Uturuki ametambulisha chapa yake mpya ya mitindo itakayo deal na utambulisho wa mtu mweusi inayoitwa ‘Black Imagination’
Happy anaeleza kuwa anataka kufuata nyayo za aliyekuwa mbunifu mkubwa wa mavazi ambaye kwa sasa nina marehemu Virgil Abroh, ambaye mara zote alisimama kitetea ngozi nyeusi kupitia kipaji chake.
Happy anadai pia ameamua kukata nywele zake ili kuendeleza kuuvaa uhusika wa Mwanamke wa Kiafrika kupitia kazi yake kwa njia ya ubunifu wa mavazi kama ilivyokuwa kwa Marehemu Virgil.