Menu ›
Burudani
Wed, 27 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mbuni aliyetoroka kwenye hifadhi ya wanyama iitwayo Bug City na kuingia barabarani katika mji wa Seongnam nchini Korea Kusini amekamatwa baada ya lisaa limoja akipishana na magari.
Mamlaka ya eneo hilo ilisema mapema leo kuwa mbuni huyo alitumia saa zima barabarani akikwepa magari kwenye barabara yenye msongamano mkubwa hali ambayo iliwashangaza madereva wengi.
Walioshuhudia walichapisha kwenye mitandao ya kijamii picha na video za mbuni huyo dume anayeitwa Tadori akiwa barabarani.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live