Kufuatia na video zinazosambaa mitandaoni zikimuonesha aliyekuwa msemaji wa Yanga, Haji Manara na aliyekuwa mke wa Dulla Makabila, Zaylissa kuhusishwa kutoka kimapenzi, mastaa mbalimbali wamejitokeza na kumtaka Makabila aongee chochote kuhusu tukio hilo.
Kupitia ukurasa wa Instagram wa Makabila ali-post picha siku ya jana akiwa hajaandika kitu chochote, ambapo mastaa mbalimbali kupitia upande wa ‘komenti’ wakimtaka msanii huyo kuongea kitu chochote
Kati ya ma-star hao ni Wolper, Rushaynah, Platform, Sophi Juakali, Simpletheboy na wengine wote wakimtaka Dulla Makabila aongee chochote kuhusiana na video hizo zinazo-trend mitandaoni.