Wasanii Rema, Burna Boy, Wizkid, Ayra Starr, Oxlade na Victony wote kutoka Nigeria wameng'ara kwenye vipengele tofauti kuwania tuzo za Muziki za Billboard 2023.
Billboard ilitoa orodha kamili ya majina ya wasanii na vipengele siku ya Alhamisi huku Rema mwimbaji wa 'Calm Down' ametajwa kuwania vipengele sita tofauti ikiwa ni pamoja na Tuzo ya Mwanamuziki Bora wa Afrobeats, Wimbo Bora wa Redio, Kolabo Bora, Wimbo Bora wa Billboard Global 200, Wimbo Bora wa Billboard Global (isipokuwa Marekani) na Wimbo Bora wa Afrobeats.
Huku wasanii wengine kutoka Nigeria waliotajwa ni Burna Boy, Tems, Wizkid, Ayra Starr, Oxlade na Victony ambao wametajwa kwenye vipengele vya Top Afrobeats na Top Afrobeat song ambavyo ni ingizo jipya katika tuzo hizo.