Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mastaa Bongo watikisa playlist ya Kamala, Mondi hayumo

Kamala Playlist Mastaa Bongo watikisa playlist ya Kamala, Mondi hayumo

Tue, 28 Mar 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris ametoa Spotify playlits yake ya nyimbo 25 za Wasanii wa Afrika ambazo anazikubali ambayo ameipa jina la “Safari Zangu: Ghana, Tanzania na Zambia”, kama sehemu ya kukuza muziki na kuwapa hamasa zaidi Wasanii wa Afrika wakati huu ambapo anafanya ziara katika Nchi hizi tatu ndani ya Wiki hii.

Mtandao maarufu wa Billboard umeitaja orodha hiyo ya Wasanii wa Nchi hizi tatu na nyimbo zao ambazo Wapenzi wa Muziki Duniani wanaweza kusikiliza kupitia Spotify na platform nyingine lengo likiwa ni kukuza Wasanii na mdundo wa Kiafrika hususani kutoka kwa Wasanii wa Ghana, Tanzania na Zambia.

Wasanii wa Tanzania ambao wamo kwenye orodha hiyo ni pamoja na Harmonize na wimbo wake mpya ambao video yake imeachiwa rasmi leo ya Single Again, pia Zuchu (Utaniua), Alikiba (Mahaba) Jay Melody (Sawa), Mbosso (Shetani), Jux & Marioo (Nice Kiss), Darassa (No Body) , Marioo & Abbah (Lonenly), Platform & Marioo (Fall).

Tayari Kamala ametua Ghana tangu jana ambapo pamoja na mengine anayoyapa kipaumbele kwenye ziara yake ikiwemo maendeleo ya kiuchumi, mabadiliko ya tabia nchi, usalama wa chakula na ongezeko la idadi ya vijana pia anatarajia kukutana na Wasanii wa Kiafrika ikiwemo wale ambapo wapo kwenye playlist yake ili kuongea nao na kuona namna bora ya kuufikisha muziki wao kwenye masoko makubwa ya muziki Marekani.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live