Kampuni ya Alcor Life Extension Foundation ya Arizona, iliyopo nchini Marekani imeanza mchakato wa kuhifadhi miili ya watu waliofariki kwa magonjwa mbalimbali kwa kuwaweka kwenye baridi kali ili ifikapo mwaka 2040 waweze kuwafufua.
Kampuni hiyo mpaka kufikia sasa imefanikiwa kuhifadhi miili 200 huku watu wengine 1,000 wakiwa tayari wamesaini mkataba kwamba pindi watakapo fariki wahifadhiwe na kampuni hiyo.
Ili kupata fursa ya kufufuliwa teknolojia hiyo itapoanza kufanya kazi mwaka 2040, kabla ya kufa utatakiwa kulipa Tsh 470 Milioni, lakini mpaka kufikia sasa bado haijabainishwa kuwa ‘teknolojia’ hiyo kama inaweza kufanya kazi .