Diamond Platinumz ni msanii maarufu wa Tanzania na miongoni mwa wasanii wa kimataifa wanaojulikana kwa kuimba kwa lugha ya mama. Diamond anamiliki rekodi kubwa zaidi nchini Tanzania, Lebo ya WCB imekuza miongoni mwa wasanii wakubwa wa Tanzania.
Hawa ni pamoja na Harmonize, Rayvanny, Richard Mavoko, Mboso, Queen Darleen na Zuchu. Mwingine aliyejipatia umaarufu kupitia lebo hiyo ni mpiga picha wa Diamond, Lukamba ambaye ameachana na lebo hiyo na sasa anafanya shughuli zake za muziki.
Hata hivyo licha ya Diamond kuwasaidia, baadhi yao wameikacha label hiyo wengine wakiwa katika hali nzuri wengine wakiwa katika hali mbaya.
Lukamba ni miongoni mwa wasanii ambao wameachana na Wasafi kwenye mahusiano ambayo si mazuri na bosi wake. Hivi karibuni baadhi ya mashabiki walimkashifu Lukamba kupitia mitandao ya kijamii wakidai kuwa hana shukrani kwa bosi wake hata baada ya kuzawadiwa gari na Diamond.
Lukamba alikuwa mpiga picha wake rasmi lakini kwa sasa aliondoka na kuanzisha kampuni yake; Lukamba aliliaa sanaa alivyopewa gari na Simba ila leo anamdharau hawa vijana hawa hawana shukrani kabisa." Shabiki mmoj aliandika.