Menu ›
Burudani
Sat, 30 Dec 2017
Chanzo: bongo5.com
Mbunifu wa mavazi, Martin Kadinda amesema kwa namna Vanessa Mdee anavyofanya muziki wake anaiweka sehemu nzuri Bongo Flava kimataifa.
Martin amesema hayo katika katika uzinduzi wa albamu mpya ya Vanessa ‘Money Mondays’ hapo jana.
“Vanessa ni msanii ambaye anafanya jitihada kujitengeneza yeye na brand yake, ukiangalia jinsi anatoa nyimbo zake kuanzia wa kwanza unaona kabisa anaelekea wapi,” amesema.
“Pili anainyanyua industry kwa ujumla anahakikisha anafanya kolabo na wasanii wakubwa, kwa hiyo international anatuweka kwenye ramani nzuri kimuziki,” amesisitiza.
Chanzo: bongo5.com