Menu ›
Burudani
Wed, 19 Apr 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Chawa maarufu na mtangazaji wa Clouds FM, Mwijaku amesema kwamba kuna bifu linafukuta kati ya wasanii wawili, Marioo na Rayvanny chanzo kikiwa ni Paula.
Mwijaku amesema, hivi karibuni wasanii hao walipokuwa kwenye bethidei ya Billnass, wasanii hao hawakusalimiana kitu ambacho anaona ni hatari.
"Hii ni hatari, hata kama ni mambo ya mahusiano kwamba Rayvanny anaumia Paula kuchukuliwa na Marioo lakini haya ndio mambo yalisababisha hata kule Marekani wasanii wakauana, ogopa sana mwanamke ndio chanzo cha uhasama popote, Basata wawasaidie," alisema Mwijaku.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live