Msanii wa Bongo Fleva, Marioo ametamba kwamba, anazo ngoma kali nyingi ambazo ameziachia na zote zinafanya vizuri hivyo siku ya shoo yake Januari 28, itakuwa balaa pale Mlimani City jijini Dar.
Marioo anatarajia kuwa na event hiyo aliyoipa jina la The Kid You Khow ambayo amesema ngoma zake zinavyotamba, baada ya siku hiyo, balaa litaendelea kwa mwaka mzima.'
"Yaani haya mangoma yalivyohit, nasemaje baada ya event yangu ya Mlimani City Jan 28 natoa angalizo kwa wasanii wenzangu tuendelee kushambulia hivi hivi na mimi mwaka huu sitawaangusha kabisa ni mamiziki na machupa makali," aliandika Marioo kwenye Insta Story yake.