Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Marioo ataka kolabo tena na Harmonize

Harmo Na Marioo.jpeg Marioo ataka kolabo tena na Harmonize

Wed, 10 Jan 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Harmonize na Marioo kwa mara nyingine tena wameonekana studioni katika kile kinasemekana wawili hao wamejumuika pamoja kufanya kolabo.

Endapo taarifa hizo ni kweli, basi hii itakuwa ni kolabo yao ya pili bada ya kolabo ya kwanza ya ‘Naogopa’ kupata ufanisi mkubwa mwaka mmoja uliopita.

Ukurasa wa Instagram wa Konde Gang ulipakia video ya Marioo na Harmonize wakiwa kwenye studio wakirekodi wimbo na kuandika kwamba wawili hao wameamua kuwabariki mashabiki wao kwa mara nyingine tena na ngoma ya pamoja.

“Mnakumbuka hii combo? OMG wanarudi tena,” ujumbe huo ulisema.

Mashabiki wa wasanii hao walisalia na maswali mengi wakijiuliza wimbo huo utakuwa ni wa maudhui gani ikizingatiwa kwamba maisha yao kwa njia moja au nyingine yamepishana katika suala zima la kimapenzi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live