Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

"Mapenzi yamenitesa,natamani kulia" - Ally Nipishe

ALIII "Mapenzi yamenitesa,natamani kulia" - Ally Nipishe

Mon, 26 Apr 2021 Chanzo: eatv.tv

Msanii wa BongoFleva Ally Nipishe amefunguka kusema mapenzi yamemtesa na yamemrudisha nyuma kupata mafanikio kutokana na mtu aliyekuwa naye kwenye mahusiano.

Ally Nipishe amesema watu wasiwashangae wasanii kuimba nyimbo za mapenzi kwani hata wao wenyewe yanawatesa japo mashabiki hawajui kitu gani kinawatokea na kinachoendelea kwao.

"Mapenzi yamenitesa na yananikumbusha mbali mpaka natamani kulia, yaliniyumbisha sana kwenye 'game' kwa sababu kipindi kile nilikuwa naanza kufanikiwa halafu mtu anakuja kunirudisha nyuma, hakuna mtu anaeweza kuyamudu mapenzi ila watu wana-maintain tu" amesema Ally Nipishe

Mengine zaidi aliyoyazungumza Ally Nipishe kuhusu kuteswa na mapenzi bonyeza hapa chini kutazama.  

Chanzo: eatv.tv